Sunday, September 19, 2010

Nguo za Lesi

Lesi ni aina ya kitambaa kinachotengenezwa kwa kuvuta vuta kitambaa kupata kitambaa cha matundu matundu chenye umbile la kupendeza...lesi inaweza kutengenezwa kwa mashine ama mkono.....









Hii picha ya mwanzo kabisa Chantal amevaa nguo ya sketi nyeusi na blausi nyeusi ya lesi















katika picha hiyo nyingine hii Chantal amevaa sketi nyeusi na blausi nyeupe iliyopitishwa lesi kwa juu...mfano imefumiwa....imependeza sana....



na hii picha Mama Biya amevalia nguo ya lesi ya kizambarau iliyotulia na kofia ya misalaba maalum kwa ajili ya Papa...







katika picha hii Madam amevaa nguo ya machungwa...na shati la lesi nyeusi...angalia jinsi nguo yake inavyotokeza kwenye shati la lesi nyekundu....ni nzuri mpaka basi....












Madam Chantal Biya anapenda sana kuvaa nguo za lesi....lesi ni kitambaa ambacho kinauzwa ghali sana madukani,na ukivaa nguo iliyotengenezwa na vitambaa hivi unapendeza sana,

katika picha hii Chantal amevaa nguo ya lesi ya kibuluu iliyotulia....amependeza sana

Saturday, September 18, 2010

MAGAUNI YA UKWELI...


Wanawake watatu wa kinaijeria wamevaa nguo ya aina moja iliyotengenezwa na Lisa lebo yake inaitwa 'Jewel'...ona hayo maduara yalivyokatwa katwa..na mfano wa dhahabu iliyo kwenye kiuno,na shingoni kumezungushiwa dhahabu,chagua mmoja wao unayeona amependeza zaidi...

HARUSI.







HARUSI YA KINAIJERIA
MMEONA JINSI WALIVYOVAA NGUO NYEUPE ZILIZOCHANGANYA NA WEUSI PAMOJA NA MCHANGANYIKO KIDOGO MWEKUNDU..NIMEPENDA SANA

Tuesday, June 29, 2010

NAMNA YA KUFUNGA 'GELE"...

GELE

'GELE" ni neno la Kiyoruba linalomaanisha matambaa ya kichwani ya wanawake,Wayoruba ni watu waishio kusini mwa Nigeria,na ni kabila kubwa kuliko yote kutoka jangwa la sahara.Wanawake wa kiyoruba wanasifika sana kwa ufungaji vilemba kichwani,japokuwa malemba yanavaliwa na karibu wanawake wengi wa kiafrika,gele sio tu ni kilemba bali ni kipaji cha sanaa.




Friday, June 25, 2010

NIMEUPENDA HUU MSHONO..


NAUTAFUTIA TU SEHEMU YA KWENDA KUUVALIA,IPO SIKU TU MTANIONA NIMETILILIA HII NGUO..MSIKAE MKASHANGAA..HIVI NI VIJIMAMBO TU.

AINA MBALI MBALI ZA MALEMBA.


HIZI NI AINA MBALIMBALI ZA KUFUNGA MALEMBA,UNAWEZA UKAFUNGA MAREFU AMA MAFUPI KUTIKANA NA WEWE UNAVYOPENDA.



AINA YA MKUFU WA KUVALIA TENGE,BABU SIO KILA MKUFU UNAVALIA TENGE,SHURTI UWE ULE MWENYEWE.